Entertainment

Koffi apagawisha mashabiki wake

 

 

MWANAMUZIKI nguli Afrika, Koffi Charles Olomide alikonga nyoyo za mashabiki wake kwenye uzinduzi wa tamasha la ‘Tusker Cannival’ lililofanyika usiku wa kuamkia jana kwenye Viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam.
Koffi alipanda jukwaani saa saba kasorobo usiku baada ya onyesho la ufunguzi zilizofanywa na bendi mbalimbali za hapa nchini.
Katika onyesho hilo lililofanywa na watu 26 akiwamo Koffi, ilikuwa yenye ubunifu mkubwa huku mwanamuziki huyo akielezea furaha yake kuweza kufika Tanzania kwa mara nyingine baada ya miaka kadhaa aliyowahi kutembelea hapa nchini.
“Nina muda mrefu kidogo sijawahi kufika Tanzania, naipenda nchi hii na nawapenda wote siwezi kusema ni namna gani nimefurahi kwani niliwakumbuka,” alisikika Koffi kabla ya kuanza onyesho hilo.
Onyesho hilo ilifunguliwa na Wazee Sugu na baadaye walifuatia Mapacha Watatu, Twanga Pepeta, Diamond Sound, Skylight Band.
Mke wa Olomide, Cindy aliimba wimbo mmoja na kumkaribisha Koffi jukwaani, na mara alipopanda jukwaa alipokelewa na shangwe nyingi ambazo zilidhihirisha kuwa mwanamuziki huyo bado yupo katika chati za muziki wa dansi Afrika.
Koffi mwenye nyimbo 281, aliwataka mashabiki wa wake wachague ni wimbo upi wanautaka kulingana na muda wake mchache jukwaani, hali iliyokuwa ngumu kwa mashabiki waliokusanyika uwanjani hapo kutoa majibu sahihi


No comments:

Post a Comment